• Kuimarisha ushirikiano wa ulinzi katika ngazi zote ili kuhakikisha kuwepo kwa usalama wa bahari.
• Kuimarisha utayari wa kukabiliana na maafa kwa kuchukua hatua thabiti na za haraka.
• Kuhamasisha kukuza uelewa, kujenga uwezo wa kiufundi na utaalamu juu ya mpango mkuu wa matumizi ya bahari.
• Kuandaa mbinu bunifu za upatikanaji wa fedha ili kusaidia kukuza Uchumi wa Buluu katika ngazi zote.
• Kuimarisha uwezo wa kufanya tafiti na maendeleo ili kuendana na mahitaji ya maendeleo ya siku zijazo.
• Kuanzisha mfumo wa usimamizi wa taarifa na takwimu za Uchumi wa Buluu unaozingatia maarifa na taasisi za utafiti na habari za Zanzibar na kutumia fursa za Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).
• Kuimarisha ushirikiano na mataifa mbalimbali kwa ajili ya kukuza Uchumi wa Buluu na Usimamizi wa Bahari.
• Kuweka hatua madhubuti za kuzuia VVU/UKIMWI na miripuko katika sekta za Uchumi wa Buluu.
• Kuimarisha uwezo kwa wanawake, vijana na watu wenye mahitaji maalum katika Uchumi wa Buluu.
• Kuimarisha ushirikishwaji wa wanawake, vijana na watu wenye mahitaji maalum katika mipango ya Uchumi wa Buluu.
• Kukuza ubunifu katika sekta za Uchumi wa Buluu kwa wanawake, vijana na watu wenye mahitaji maalum.
• Kuboresha upatikanaji wa soko kwa wanawake, vijana na watu wenye mahitaji maalum katika Uchumi wa Buluu.