Mnamo mwaka 2016 Baraza la Wawakilishi Zanzibar liliandika historia mpya ya Zanzibar baada ya kupitisha Sheria Nambari 6 ya Mwaka 2016 Sheria ya Mafuta na Gesi Asilia Zanzibar. Sheria hii inayosimamia na kutoa miongozo ya utafutaji na uchimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia pamoja na mambo mengine imeanzisha taasisi muhimu katika Sekta ya Mafuta na Gesi Asilia ikiwemo Kampuni ya Maendeleo ya Mafuta na Gesi Asilia Zanzibar.